Parliament Logo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Baraza la Sanaa la Taifa

Historia

Historia

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) ni Shirika la umma lililoundwa kwa Sheria ya Bunge Na. 23 ya Mwaka 1984 kama ilivyofanyiwa marekebisho na Sheria Na. 5 ya Mwaka 2019. Historia inaonyesha kuwa, Sheria ya kuunda upya Baraza hili ilifanywa kwa kuunganishwa Sheria ya Baraza la Sanaa la Taifa ya Mwaka 1974 na Baraza la Muziki la Taifa (BAMUTA) ya Mwaka 1974. Baraza liliundwa ili lisimamie maendeleo ya sanaa nchini


Kazi za Baraza

Kwa mujibu wa Sheria Na. 23 ya mwaka 1984 kama ilivyofanyiwa marekebisho na Sheria Na. 5 ya Mwaka 2019, ambayo kwayo Baraza liliundwa, Majukumu ya Baraza ni pamoja na :

  • Kufufua na kuhimiza maendeleo ya kazi za Sanaa
  • Kufanya tafiti wa masuala mbalimbali ya Sanaa
  • Kutoa ushauri na misaada ya kitaalamu kwa asasi au watu wanaojihusisha na shughuli za sanaa.
  • Kuratibu shughuli za sanaa zinazofanywa na watu au Taasisi mbalimbali
  • Kutoa na kuimarisha mipango ya mafunzo kwa Wadau wa Sanaa
  • Kuishauri Serikali juu ya mambo yahusuyo maendeleo na uzalishaji wa kazi za Sanaa.
  • Kuhamasisha maendeleo ya Sanaa kwa njia ya Maonyesho, Mashindano, Matamasha, Warsha na Semina.
  • Kuanzisha, kukusanya na kuhifadhi torwi, ikiwa pamoja na zile zinazohusu watu, Asasi, Taasisi, vifaa na miundo mbinu inazohusiana na Sanaa
  • Kusajili Wasanii na wale wote wanaojihusisha na shughuli za Sanaa


Muundo wa Baraza

Baraza la Sanaa la Taifa lina wajumbe wa Baraza ambao uteuliwa na Waziri anayehusika na masuala ya Sanaa. Mwenyekiti wa Baraza uteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mwenyekiti pamoja na wajumbe wa Baraza uteuliwa kwa kipindi cha miaka mitatu. Wakati ambapo vipindi vya kuteuliwa kwa wajumbe havina ukomo, uteuzi wa Mwenyekiti wa Baraza ni kwa vipindi viwili tu vinavyofuatana. Kwa kawaida wajumbe wa Baraza uteuliwa kwa msingi wa uwakilishi wa mikoa, asasi, asasi zinazofundisha Sanaa, idara za Serikali na asasi zisizo za Serikali.


 

Baraza linaongozwa na Katibu Mtendaji, ambaye ndiye Afisa mtendaji mkuu. Baraza lina idara Mbili zifuatazo:

  • Idara ya Ukuzaji na Maendeleo ya Sanaa, inayohusika na huduma za Sanaa
  • Idara ya Huduma ya Taasisi, inayohusika na shughuli za huduma za Taasisi


 

Licha ya idara hizo Mbili, kuna vitengo vitano ambavyo hufanya kazi moja kwa moja chini ya Katibu Mtendaji. Vitengo hivyo ni ;

  • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
  • Kitengo cha Manunuzi
  • Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma
  • Kitengo cha Huduma za Sheria
  • Kitengo cha TEHAMA na Takwimu

Sanaa hujumuisha

  • Muziki

Ambao unaweza kuwa wa kuimba na wa vyombo uliorekodiwa kwa sauti au utunzi wa muziki ulioandikwa, bendi, muziki wa jazi, ala, uliorekodiwa, video, taarabu, kwaya, gwaride,muziki wa asili wa ngoma na unaoambatana na maigizo na thamthiliya.

  • Sanaa za Ufundi

Hujumuisha picha za kuchorwa kwa rangi, uchoraji wa kawaida, michoro ya majalada, vitabu au magazeti, uchoraji wa kwenye vitu vigumu kama metali au mbao, uandishi wa herufi ulionakishiwa, sanaa za vikaragosi kwa kutumia kompyuta na michoro iliyochapishwa. Ramani, michoro ya majengo na vielelezo, sanaa za kuumba na kuchonga, picha mgando za kamera, Kazi za usanifu majengo katika maumbo Sanaa za viwandani ikiwa pamoja na zilizo katika picha au zilizofumwa na urembo, na ubunifu wa mavazi, ususi na useketaji wa nguo.

  • Sanaa za Maonyesho

Michezo ya kuigiza ya jukwaani, maigizo bubu, usanifu wa majukwaa, maleba, mapambo, uandishi wa tamthiliya, ngoma na ubunifu wake, sauti na vifaa vya jukwaani, sarakasi za binadamu au za wanyama, michezo ya redio.

Settings