News

WAZIRI NDUMBARO ASISITIZA BASATA IENDELEE KUSIMAMIA MAADILI

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amefanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Bodi ya Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Prof. Saudin Mwakaje Oktoba 6, 2023 Jijini Dar es Salaam

WAFANYAKAZI WA BASATA KATIKA SHEREHE YA SIKU YA WAFANYAKAZI 2023

Wafanyakazi wa Baraza wakisherehekea siku ya wafanyakazi Duniani na kutoa ujumbe wenye kuonyesha kaulimbiu ya sherehe hiyo

MHE. MWIJUMA AFANYA KIKAO NA BARAZA

Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Hamis Mwijuma akiwa katika kikao na Menejimenti ya Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) makao makuu ya Baraza yalipo Kivukoni Jijini Dar es Salaam

MHE. MSIGWA APOKELEWA KWA SHANGWE WAKATI AKIWASILI BASATA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Gerson Msigwa apokelewa Baraza mara baada ya kuwasili katika matembezi yake kwa Taasisi zilizopo chini ya Wizara

KATIBU MTENDAJI WA BARAZA KATIKA KILELE CHA TUZO ZA MUZIKI TANZANIA 2022

Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Dkt. Kedmon Mapana akitoa taarifa kwa Wadau wa Sanaa na Wasanii maendeleo ya mazuri ya Tuzo za Muziki Tanzania

Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Dkt. Kedmon Mapana akicheza ngoma ya Spot katika uzinduzi wa Sanaa mtaa kwa mtaa

Mwanafunzi Msanii Mussa H. Mbonde kutoka shule ya msingi ya Siasa Utete akitumbwiza katika uzinduzi wa Sanaa mtaa kwa mtaa

Kikundi cha ngoma cha Urugwayi kutoka Rufiji kikitumbwiza wakati wa uzinduzi wa Sanaa mtaa kwa mtaa

Kikundi cha uchongaji kutoka Ikwiriri Wilaya ya Rufiji wakimkabidhi Katibu Mtendaji wa BASATA Dkt. Kedmon Mapana zawadi ya Sanaa ya Uchongaji

Uzalishaji wa kazi za Sanaa ya Vinyago kutoka kwa Wasanii wa Sanaa za uchongaji Rufiji

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) ni Shirika la umma lililoundwa kwa Sheria ya Bunge Na. 23 ya Mwaka 1984 kama ilivyofanyiwa marekebisho na Sheria Na. 5 ya Mwaka 2019. Historia inaonyesha kuwa, Sheria ya kuunda upya Baraza hili ilifanywa kwa kuunganishwa Sheria ya Baraza la Sanaa la Taifa ya Mwaka 1974 na Baraza la Muziki la Taifa (BAMUTA) ya Mwaka 1974. Baraza liliundwa ili lisimamie maendeleo ya sanaa nchini


Dira

Kuwa chombo chenye uwezo wa hali ya juu wa kutoa huduma bora kitaifa katika maendeleo ya sanaa


Lengo kuu

Kufufua, kukuza na kuongeza maendeleo ya utengenezaji wa kazi bora za Sanaa.


Maadili

Maadili ya msingi ya Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) ni kuhimiza na kukukuza utamaduni halisi wa sanaa ya Kitanzania, kudumisha ubobezi na ubora wa hali ya juu na kuchochea ubunifu na uvumbuzi katika sanaa

  • Limepania kuhimiza na kukuza utamaduni halisi wa sanaa ya Kitanzania
  • Limepania kudumisha ubobezi na ubora wa hali ya juu
  • Limepania kuhimiza ubunifu na uvumbuzi katika sanaa

Copyright © 2021. All Rights Reserved.